Home
 
Banner
Karibu Gazeti la Majira (Gazeti huru la kila siku)
G7 yahahidi kusamehe madeni Haiti PDF Print E-mail
Monday, 08 February 2010 07:50

Iqaluit, Canada


WATU zaidi ya milioni nchini Haiti wanahitaji msaada, nchi zilizoendelea  kiviwanda zimesema kuwa zinaifutia madeni nchi hiyo, kutokana na  janga walilopata la tetemeko la ardhi lililosababisha vifo, watu kukosa makazi na kuharibika kwa miundombinu mwezi uliopita.

Read more...
 
Watu 40 wafa kwa bomu Iraq PDF Print E-mail
Monday, 08 February 2010 07:47

BAGDAD, Iraq


MABOMU mawili ya kujitoa mhanga yameua watu kiasi cha 40 na kusababisha wengine zaidi ya 140 kujeruhiwa, katika tukio lilitokea nje ya mji wa Karbala, nchini Iraqi  juzi, taarifa ya polisi imesema.

Read more...
 
Sitta awasifu marais wastaafu PDF Print E-mail
Monday, 08 February 2010 07:46
Na Mwandishi Wetu

SPIKA wa Bunge, Bw. Samuel Sitta ameonesha kukerwa na watu wanaowaponda warais wastaafu kwa madai kuwa hawaitakii mema Tanzania.
Read more...
 
Kura za pesa zasumbua CCM PDF Print E-mail
Monday, 08 February 2010 07:44

  • Pinda aungana na JK kupinga 'uongozi kwa pesa'
  • Ataka wanachama kuwachuja wanaonunua wananchi
  • Wabunge wauhofia mswada wa fedha za uchaguzi

Na Mwandishi Maalumu, Dodoma

 
WAZIRI MKUU Mizengo Pinda amesema ni lazima Chama cha Mapinduzi (CCM) kiwakatae watu wanaotumia fedha kutafuta nafasi za uongozi kwani viongozi wa aina hiyo wakipita
serikali itajikuta ina viongozi wasiofaa ila wako pale kwa sababu tu wana pesa.
 
Ametoa kauli hiyo jana jioni wakati akiwahutubia wakazi wa Wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma, kwenye maadhimisho ya miaka 33 ya kuzaliwa kwa CCM yaliyofanyika kimkoa wilayani humo.
 
Alisema CCM iliangalia utaratibu unaotumika katika kupitisha viongozi na kubaini kuwa kuna kasoro ndipo ikafikia uamuzi wa kubadili mfumo huo ili wanaogombea ubunge na udiwani waende kupigiwa kura kuanzia katika ngazi ya tawi.
 
Alisema uamuzi huo mpya unatoa nafasi kwa wananchi kuamua kama mgombea anawafaa au hawafai na kwamba endapo watabaini kuna watu ambao wanakuja kwa staili ya ‘mkao wa
kula’ waamue kusema hapana mara moja.
 
“Kama kuna mtu anakuja na staili ya mkao wa kula ni lazima wote tuseme hapana, la sivyo tutakuwa na viongozi wasiofaa na wako madarakani eti kwa sababu tu wana pesa
na walitumia pesa zao kuhonga wananchi,” alisisitiza.
 
“Ni lazima Chama kikatae kuwapitisha watu wa aina hii... muanze kuwachuja tangu wilayani na wala hakuna haja ya kuwaleta kwenye Kamati Kuu... haiwezekani kuwa na
viongozi ambao wanawanunua kwa sh. 5,000/- au sh. 20,000/-,” alisema.
 
“Kama chama ni lazima tuendelee kukataa wenye tamaa ya mali kupindukia kwa sababu matokeo yake ni kujikuta tuna watu wenye kula rushwa...huwa najiuliza sababu za
watu kujilimbikizia mali kupita kiasi wakati mwisho wetu wote ni kichumba cha pembe nne,” alisema.
 
Alisema Watanzania wasikubali kuwa na viongozi wenye kupenda kujilimbikizia mali kwa sababu mwisho wa yote watatumia nafasi hizo kuhonga, ili kupata tenda na mikataba
mikubwa.

“Haiwezekani kiongozi upende kujilimbikizia mali ili upate umaarufu tu, ni lazima utatumia utajiri huo kuhonga ili kupata kandarasi na mikataba mikubwa,” alisema huku akishangiliwa na wakazi hao.
 
Alionya kwamba ili kutibu ugonjwa huo wa kuwa na viongozi wenye kupenda mali, vyama vya siasa havina budi kurudi kwenye chaguzi za vyama vyao. “Lazima turudi kwenye
vyama vyetu ili kutibu ugonjwa huu, mkiwa na viongozi wachafu siyo rahisi kuunda serikali iliyo safi.”
 
Alisema japokuwa suala la rushwa ni la mtu mmoja mmoja, lakini kila chama hakina budi kusema kinachukua hatua gani dhidi ya huyo mtu mmoja mmoja, ili kuepusha tabia
hii miongoni mwa wagombea nafasi za uongozi.
 
Mtanzania ateuliwa kuwa Balozi wa Papa Sao Tome PDF Print E-mail
Monday, 08 February 2010 07:42
Na Theonestina Juma, Bukoba
 
KIONGOZI wa Kanisa Katoliki Duniani, Papa Benedict wa XVI amemteua padri wa kwanza Mtanzania, Monsignor Novatus Rugambwa (52) kuwa Askofu Mkuu na balozi wake katika visiwa vya Sao Tome na Principe.
Read more...
 
«StartPrev12345678910NextEnd»

Page 1 of 509
 

Polls

Kuachiwa huru Zombe na wenzake haki imetendeka?
 

Who's Online

We have 152 guests online

Matangazo

Tangaza nasi leo kwa gharama nafuu zaidi:
Banner
Banner
Banner
Banner